Watu watano wameuawa na wengine 96 kujeruhiwa kwenye maandamano yaliyofanywa jana kwenye jimbo la wakurdi nchini Iraq, wakati hasara ya umma ikiendelea kuenea kutokana na mishahara isiyolipwa na ufisadi. Msemaji wa ofisi ya afya ya mji wa Rania Bw. Taha Mohammed amesema vifo na majeruhi hao vimetokea mjini Rania baada ya vikosi vya usalama kufyatulia risasi na kutumia mabomu ya machozi dhidi ya waandamanaji waliochoma moto ofisi za vyama vya wakurdi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |