Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi jana alifanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Russia Bw. Sergei Lavrov, kujadili uhusiano kati ya nchi zao na hali ya peninsula ya Korea. Mawaziri hao pia walibadilishana maoni kuhusu masuala ya kimataifa yanayofuatiliwa kwa pamoja na nchi zao, na kuahidi kudumisha mawasiliano ya kimkakati kuhusiana na masuala makuu duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |