Korea Kaskazini imekana ripoti zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari vya Marekani zinazoishutumu nchi hiyo kutekeleza mpango wa kuendeleza silaha za kibaiolojia, ikiwa ni sehemu ya juhudi za nchi hiyo kuongeza uwezo wake wa silaha za maangamizi. Taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini imezitaja shutuma hizo kama mfano mwingine wa tabia ya Marekani ya kupotosha ukweli wa mambo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |