• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Hamilton ajikaanga kwa mafuta yake mwenyewe Mercedes

    (GMT+08:00) 2017-12-21 09:40:17

    Lewis Hamilton kwa sasa anaweza akawa hana furaha kubwa baada ya kitumbua chake kuonekana kuingia mchanga. Dereva huyo wa magari ya mashindano ya Langa Langa kutoka Mercedes ameonekana kusambaza picha ya gari lake la kifahari aina ya LaFerrari kitendo ambacho kimekuwa kikizua maswali mengi. Hali hiyo inatokana na kampuni ya Mercedes kuwa na upinzani mkubwa na Ferrari ambayo dereva wake katika mashindano ya magari ya Langa Langa ni Sebastian Vettel. Gari la LaFerrari linatajwa kuwa na thamani ya kiasi cha dola milioni moja. Mastaa wengine ambao wanamiliki gari kama hilo ni Floyd Mayweather na Justin Bieber.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako