Mjumbe wa taifa wa China Bw. Yang Jiechi Jana alikutana na Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania Bw. Augustine Mahiga.
Wakati wa mazungumzo hayo, Bw. Yang amesema China itafanya juhudi katika kuimarisha mawasiliano kati yake na Tanzania katika sekta mbalimbali, kuongeza nguvu katika kubadilishana uzoefu kuhusu mambo ya utawala, kuimarisha uaminifu wa kisiasa na uratibu katika mambo ya kikanda na ya kimataifa.
Naye Bw. Mahiga amefurahishwa wa pendekezo la China la "Ukanda mmoja, Njia moja" na mtizamo wa maendeleo, pia alieleza matumaini ya Tanzania ya kuwa mwenzi mzuri wa ushirikiano wa China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |