Bingwa wa Afrika Mashariki na kati Gabriel Ochieng ametumia sekunde 236 kumuangusha kwa knockout Joseph Akhahoya na kushinda pambano amablo halikuwa la ubingwa wowote lililofanyika jana mjini Nairobi.
Ochieng ambaye amerejea baada ya kupoteza katika mapambano ya kutafuta ubingwa wa WBA kanda ya Afrika, alimpa nafasi Akhahoya ya kumaliza raundi ya kwanza kabla ya kummaliza katika sekunde ya 56 ya raundi ya pili.
Pambano hilo lililoandaliwa na Team Boxing Promotion lilihudhuriwa na mwenyekiti wa Baraza la linalosimamia ngumi za kulipwa nchini Kenya KPBC Bw. Reuben Ndolo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |