• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa apongeza uchaguzi mkuu wa amani nchini Liberia

    (GMT+08:00) 2017-12-28 09:27:27

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kwamba Bw Antonia Guterres amepongeza duru ya pili ya uchaguzi mkuu wa Liberia uliofanyika Jumanne kwa amani.

    Msemaji wa umoja wa mataifa ameongeza kuwa Bw Guterres amemtuma kiongozi wa zamani wa Nigeria Bw Olusegun Obasanjo kushuhudia makabidhiano ya kwanza ya madaraka ya amani nchini Liberia katika kipindi cha zaidi ya miaka 70. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka maoni ya wapiga kura yaheshimiwe, na makabidhiano hayo ya madaraka yafanyike kama ilivyopangwa.

    Duru ya pili ya uchaguzi mkuu ilifanyika Jumanne, na mvutano ulikuwa ni kati ya makamu wa rais Joseph Boakai na mcheza soka wa zamani wa George Weah.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako