Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF limekanusha taarfia zinazosambaa zikipotosha kauli ya Rais Wallace Karia kuhusu kuzuia mashindano ya soka yasiyo rasmi. Taarifa ya TFF imeeleza kuwa watu wanamnukuu vibaya Rais Karia kwani hakusema shirikisho hilo linafuta mashindano bali zinaandaliwa kanuni ambazo zitatakiwa kufuatwa na waandaaji wa mashindano hayo.
Kwa mujibu wa taarifa TFF inaandaa kanuni ili mashindano yote ya aina hiyo yakidhi vigezo katika utaratibu mzuri na watapata vibali kupitia FA Wilaya na Mikoa baada ya kutimiza vigezo vitakavyowekwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |