Waziri wa mambo ya nje wa Palestina Bw. Riad Malki amesema mamlaka ya taifa ya Palestina PNA itatoa wito kwenye mkutano wa kilele wa jumuiya ya nchi za kiarabu, kususia nchi zitakazohamisha balozi zao nchini Israel kwenda Jerusalem. Mapema wiki hii, nchi wanachama 138 wa Umoja wa mataifa zilipiga kura na kupitisha azimio la kukataa mabadiliko yoyote kwa hadhi ya Jerusalem, ambalo limeupinga uamuzi uliotolewa Desemba sita na rais Donald Trump wa Marekani wa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |