Rais Vladimir Putin wa Russia amesema, mlipuko uliotokea jumatano kwenye supamaketi moja mjini St. Petersburg nchini humo ni shambulizi la kigaidi.
Rais Putin ameagiza Idara ya usalama FSB kuwakamata magaidi haraka iwezekanavyo, na kwamba endapo maofisa wa usalama watakabiliwa na hatari ya maisha kwenye operesheni ya msako, wamepewa mamlaka ya kuwaangamiza magaidi papo hapo bila haja ya kuwakamata hai.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |