Watu 36 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika ajali ya barabarani magharibi mwa Kenya.
Ajali hiyo ilitokea alfajiri baada ya basi na lori kugongana katika eneo zilikotokea ajali nyingi katika barabara kuu ya Nakuru-Eldoret.
Polisi wamesema basi hilolilikuwa limebeba abiria kwenda Nairobi wakitokea mji wa mpakani wa Busia huku lori likielekea kwenye mji wa Eldoret kaskazini magharibi mwa Kenya.
Mkuu wa upelelezi katika jimbo la Rift Valley Gideon Kibunja amesema basi hilo lilizidisha abiria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |