• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soka, Matokeo ligi kuu ya Uingereza, Man United warejea nafasi ya pili

    (GMT+08:00) 2018-01-02 10:28:07
    Manchester United wamefanikiwa kurejea katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ya uingereza baada ya kuwafunga Evertonkwa magoli 2-0.

    Magoli ya United katika mechi hiyo yalifungwa na Anthony Martial kunako dakika ya 57 na goli la pili likifungwa na Jesse Lingard katika dakika ya 81.

    Katika matokeo ya mechi nyingine iliyofanyika jana Liverpool imeendeleza wimbi la ushindi ilipowafunga Burnley kwa magoli 2-1 na magoli yao yakifungwa na Sadio Mane na Ragnar Klavan , huku goli pekee la Burnley likifungwa na Johann Gudmundsson.

    Sasa Manchester United wanasubiria matokeo ya mchezo kati ya Arsenal na Chelsea utakaopigwa siku ya Jumatano ambapo kama Chelsea atafungwa watabaki nafasi ya pili lakini Chelsea akishinda United watarudi katika nafasi ya tatu .

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako