Magoli ya United katika mechi hiyo yalifungwa na Anthony Martial kunako dakika ya 57 na goli la pili likifungwa na Jesse Lingard katika dakika ya 81.
Katika matokeo ya mechi nyingine iliyofanyika jana Liverpool imeendeleza wimbi la ushindi ilipowafunga Burnley kwa magoli 2-1 na magoli yao yakifungwa na Sadio Mane na Ragnar Klavan , huku goli pekee la Burnley likifungwa na Johann Gudmundsson.
Sasa Manchester United wanasubiria matokeo ya mchezo kati ya Arsenal na Chelsea utakaopigwa siku ya Jumatano ambapo kama Chelsea atafungwa watabaki nafasi ya pili lakini Chelsea akishinda United watarudi katika nafasi ya tatu .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |