Uchumi wa Morocco umeshuhudia ukuaji wa asilimia 3.9 katika robo ya nne ya mwaka jana, ikilinganishwa na asilimia 1 ya mwaka 2016. Kamisheni ya mipango imesema ukuaji huo ulitokana na ongezeko la asilimia 14.2 kwenye uzalishaji wa kilimo, ikilinganishwa na kupungua kwa asilimia 13.7 za mwaka 2016. Uchumi wa Morocco uliathiriwa vibaya na ukame mkali ulioanza mwaka 2015, na kusababisha hasara kubwa kwenye sekta ya kilimo katika mwaka 2016.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |