Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amelaani vikali mashambulizi yaliyotokea kwenye sherehe za mwaka mpya ambayo yamesababisha vifo na majeruhi ya watu wengi, na kuyataja mashambulizi hayo kuwa yanapaswa kulaaniwa na hayakubaliki.
Mapema ya jumatatu, watu wenye silaha wasiojulikana waliwaua mtawala wa eneo la Sanga la jimbo la Kaduna na mke wake. Vilevile katika eneo la Omoku la jimbo la Rivers, watu wasiojulikana waliwaua watu wasiopungua 16 wakiwemo wanawake na watoto, wakiwa njiani kurudi nyumbani kutoka kanisani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |