Rais Museveni ameyasema hayo wakati alipokutana na kupata chakula cha mchana na wanamichezo ambapo amesisitiza kuwa yafaa kuwe na bajeti yenye malengo kwa ajili ya kuendeleza soka na timu ya taifa, ambapo amesisitiza kuwa wachezaji wanahitaji matunzo hivyo ni jukumu la FUFA kuhakikisha hilo linatekelezeka.
Museveni pia ameahidi kuwa serikali itanunua basi jipya kwa ajili ya timu ya taifa ya mpira wa miguu.
Katika hatua nyingine, amesema serikali imeandaa fedha kwa ajili ya kulipa familia za waathirika wa ajili ya mwaka 2015 baada ya basi lililokuwa limebeba wachezaji wa timu ya taifa kugongana na basi dogo lilikuwa limebeba abiria.
Takribani shilingi billion moja, fedha za Uganda zimeandaliwa kwa ajili ya kulipa fidia kwa wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo pamoja na familia za waliopoteza maisha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |