Wenger alikasirika baada ya mwamuzi Mike Dean kuwapa West Brom mkwaju wa penalti, ambapo walifunga na kusawazisha.
Inadaiwa kwamba, aliyoyafanya Wenger katika chumba cha kubadilishia mavazi cha waamuzi baada ya mechi yalikuwa matusi na ya kukera huku akionyesha kutilia shaka maadili na uwezo wa mwamuzi.
Kufuatia shitaka hilo, Wenger amepewa nafasi ya kujitetea hadi ifikapo ijumaa saa kumi na mbili za jioni kwa saa za Uingereza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |