Huduma ya intaneti yenye kasi ya 4g sasa inaweza kupatikana katika wilaya zote nchini Rwanda.
Shirika la KT Rwanda Network, linasema mtandao wa 4G sasa unafikia asilimia 95 ya maeneo yote ya Rwanda ikilinganishwa na mwaka 2014 ambapo huduma hiyo ilikuwa ni asilimia 17 tu.
Mkurungezi wa 4G Square John Ntwali Ndorimana, amesema hatua hiyo itawezesha biashara na mawasiliano kufanyika kwa haraka.
Kulingana na taakwimu matumizi ya simu za mkononi nchini Rwanda yameongezeka hadi asilimia 75.5 kufikia mwezi Nove,ba mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |