Msemaji wa jeshi la Libya Bw. Ahmed Mismari amesema askari zaidi ya elfu tano wameuawa kwenye mapambano dhidi ya ugaidi mjini Benghazi, mashariki mwa Libya. Alhamisi iliyopita jeshi la Libya lilitangaza kutwaa udhibiti wa maeneo yote ya Sidi Ekhrebish katikati ya mji wa Benghazi, ambayo ni ngome ya mwisho ya magaidi mjini humo, hatua ambayo inamaanisha kuwa operesheni zote za kijeshi zilizodumu kwa miezi mitano mjini humo zimemalizika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |