Leopards maarufu Ingwe wamepangiwa kucheza na FOSA Juniors ya Madacascar katika mechi ya kombe la CAF, lakini wanahitaji kiasi cha Sh30 milioni kugharamia mikondo yote miwili, pesa ambazo mwenyekiti wao, Dan Mule amesema haziwezi kupatikana bila usaidizi wa SportPesa ambao ndio wadhamini wao wakuu. Serikali imeingia vitani na SportPesa kutokana na uamuzi wake wa kuzitaka kampuni zote za kamari nchini zitozwe asilimia 35.
Mahasimu wao wakuu, Gor Mahia ambao watawakilisha taifa katika michuano ya klabu bingwa Afrika, pia wanakabiliwa na shida hiyo kwa vile SportPesa ndio wadhamini wao. K'Ogalo wamepangiwa kucheza na Leones Vegetarianos ya Equatorial Guinea katika raundi ya kwanza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |