Hamad: Siwezi kubeza mapinduzi
(GMT+08:00) 2018-01-05 08:57:27
Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Hamad Rashid Mohammed, amesema hawezi kuyabeza mapinduzi ya Zanzibar licha ya kwamba anatoka chama cha upinzani cha Alliance Democratic Change (ADC). Alisema anaelewa umuhimu wa mapinduzi hayo ya mwaka 1964 ambayo ni mkombozi kwa wazanzibari na ni dira ya maendeleo kwa wananchi.