Wakazi wa Tehran, mji mkuu wa Iran jana wamefanya maandamano, na kutoa wito wa kuunga mkono serikali, na kupinga vitendo vya kimabavu na kuingiliwa na nchi za nje.
Baadhi ya wakazi wa mji wa Tehran walikusanyika katika misikiti na sehemu nyingine za wazi, wakitoa wito huo kuwahimiza wananchi wa Iran washikamane.
Kutokana na mfumuko wa bei, maandamano makubwa yametokea hivi karibuni katika sehemu mbalimbali nchini Iran, na vurugu zilizotokea katika maandamano hayo zimesababisha vifo na watu wengine kujeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |