• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bunge la Afrika Kusini kupitia upya kanuni za kumwondoa rais madarakani

    (GMT+08:00) 2018-01-08 09:33:46

    Bunge la Afrika Kusini limesema, litajadili daftari la utaratibu kuhusu kumwondoa rais Jacob Zuma madarakani.

    Mwishoni mwa mwaka jana mahakama ya kikatiba ilitoa hukumu kuwa bunge lilishindwa kuweka kanuni mwafaka za kumwajibisha Rais Jacob Zuma na kashfa ya Nkandla, ambapo Rais Zuma alituhumiwa kutumia vibaya fedha za umma zipatazo dola za kimarekani milioni 20 kwa ajili ya kuimarisha usalama nyumbani kwake Nkandla, katika jimbo la KwaZulu-Natal.

    Mahakama hiyo ililitaka bunge la Afrika Kusini litunge kanuni bila kuchelewa ili kuanzisha utaratibu kwa mujibu wa kifungu cha 89 cha katiba.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako