Serikali ya Libyainayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa leo imetangaza kumalizika kwa operesheni ya kijeshi iliyoanza kutekelezwa siku chache zilizopita kwenye eneo la Abu-Kammash ili kulinda usalama na kupambana na shughuli za magendo.
Serikali ya Libya imetoa amri kwa idara husika kuchukua udhibiti wa eneo la mpaka kati ya Libya na Tunisia, na imesema itahakikisha inachukua hatua za kulinda usalama wa eneo hilo na kurejesha maisha ya kawaida na inafanya juhudi zote kuwakamata wahalifu na wale wanaohatarisha maisha ya wananchi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |