Morocco na Malawi zimekubaliana kuimarisha ushirikiano kwenye sekta ya kilimo. Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Malawi Bw. Emmanuel Fabiano, na katibu wa nchi wa Morocco anayeshughulikia maendeleo ya vijijini, maji na misitu wa Morocco Bw. Hamou Ouhelli wamesema baada ya kukutana kuwa nchi hizo mbili zimehitimisha makubaliano mawili ya kuimarisha ushirikiano wa kilimo, na kuyataja kuwa ni fursa ya kutafuta njia za kuhimiza ushirikiano wa pande mbili kwenye sekta ya kilimo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |