Benki ya Dunia jana imetoa makadirio ya ongezeko la uchumi la nchi za Afrika katika mwaka 2018, na kukadiria kuwa kiasi cha ongezeko la uchumi kwenye eneo la kusini mwa Sahara barani Afrika kitafikia asilimia 3.2.
Ripoti ya benki hiyo kuhusu mustakabali ya uchumi wa dunia imeeleza kuwa, kiasi cha ongezeko la uchumi la wastani kwenye nchi 43 za Afrika zilizoko kusini mwa Sahara kilizidi asilimia 0.1 kuliko kiasi cha ongezeko la uchumi la wastani la dunia. Benki hiyo imesema ongezeko hilo linakadiriwa kuimarika katika mwaka 2018 kutokana na kuboreshwa kwa ustawi wa biashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |