Kocha mkuu wa Chelsea, Antonio Konte, amesema sare hiyo inawapa changamoto kuelekea mechi ya marudio watakapokuwa ugenini kwani watalazimika kucheza kama fainali ili kusawazisha makosa ya mechi ya jana.
Timu hzio zinatarajiwa kurudiana Januari 23, na Chelsea wanasaka kwa udi na uvumba kombe hilo ambalo hawajakuwa na bahati nalo, huku Arsenal nao wakiamini kuwa ndilo tumaini pekee lililobaki, kutokana na nafasi kuwa finyu katika ligi kuu, hukuwakiwa wameondolewa kwenye mashindano ya kombe la FA.
Mshindi wa mechi ya nusu fainali hii atakutana na mshindi wa nusu fainali nyingine kati ya Manchester City na Bristol City.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |