• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Reli ya SGR iliyojengwa na China yatajwa kuhimiza biashara ya Afrika Mashariki

    (GMT+08:00) 2018-01-11 09:35:15

    Mkurugenzi mtendaji wa Baraza la Biashara la Afrika Mashariki EABC Bibi Lilian Awinja, amesema Reli ya SGR ya Kenya iliyojengwa na China inahimiza biashara kati ya nchi za Afrika Mashariki na sehemu nyingine duniani.

    Bibi Awinja amesema, reli hiyo inayotoka Mombasa hadi Nairobi imewarahisishia wafanyabiashara nchini Sudan Kusini, Uganda na Kaskazini mwa Tanzania kusafirisha bidhaa zao na kupokea bidhaa kutoka sehemu nyingine duniani.

    Bibi Awinja amesema hayo kwenye mkutano na wanahabari kuhusu hafla ya kutoa tuzo ya Baraza la Biashara la Afrika Mashariki, huku akisema reli hiyo imepunguza muda na gharama za usafirishaji bidhaa kwenye kanda ya Afrika Mashariki.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako