• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya:Wizara ya afya yapiga marufuku uuzaji wa dawa kifua

    (GMT+08:00) 2018-01-11 19:43:17

    Bodi ya dawa na sumu imepiga marufuku uuzaji wa dawa za kukohoa katika maduka ya uuzaji wa dawa kaunti ya Mandera.

    Hatua hii inajiri baada ya bodi hiyo kugundua utumiaji mbaya wa dawa hizo zilizo na madini ya codeine yanayoweza kusababisha uraibu.

    Kulingana na Anthony Toroitich mwanchama wa bodi hiyo,Matumizi ya dawa za benylin katika kaunti hiyo yameongezeka kutoka uniti elfu 20 hadi 437,000 kutoka mwezi January hadi Novemba mwaka jana ikiwa ni ongezeko la asilimia 1000.

    Dawa hizo sasa zitauzwa chini ya masharti ya madaktari pekee.

    Matumizi ya kupita kiasi ya dawa hizo husababisha hali ya kisunzi na ulevi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako