• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mechi ya ligi kuu Marekani yapelekwa mjini London nchini Uingereza

    (GMT+08:00) 2018-01-12 10:21:50
    Timu ya Bolton Celtics imeifunga Philadelphia 76ers kwa alama 114-103 jana usiku katika mechi ya ligi kuu ya kikapu nchini Marekani lakini iliyochezwa jijini London nchini Uingereza katika mpango wa kuupeleka mchezo huo kwa mashabiki walioko nje ya Mareakani. (NBA's Global Games Series)

    Kylie Irving alipata alama 20 na Jaylen Brown 21 ambazo kwa ujumla ndizo zilizoibeba Celtics kwenye mechi hiyo.

    Lakini kivutio kikubwa kwenye mechi hiyo ilikuwa ni mahudhurio ambayo kwa kiasi kikubwa watu maarufu barani ulaya ndiyo walihudhuria wakiwemo wachezaji wa mpira wa miguu.

    Miongoni mwa watu wenye ushawishi mkubwa ni Mzee Alex Ferguson, pamoja na karibu nusu ya wachezaji wanaotikisa katika ligi kuu ya soka ya nchini Uingereza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako