Akizungumza na na waandishi wa habari, Bw Tizeba amewataka wafanyabiashara wasimamiwe ili wasiuze kinyume na bei elekezi, lakini pia hakuna sababu ya kuwaumiza wasafirishaji wakubwa kwa sababu na wao wanahitaji kupata faida.
Mapema mwaka jana, serikali kupitia iliyokuwa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, ilitangaza utaratibu wa kuagiza mbolea kwa pamoja na kuweka bei elekezi katika mbolea za kupandia na kukuzia, ambapo mbolea ya DAP haitakiwi kuuzwa zaidi ya shilingi 56,000 na UREA isizidi shilingi 48,000.
Aidha, bei hiyo elekezi inatofautiana na maeneo kulingana na umbali kutoka jijini Dar es Salaam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |