Uturuki na Somalia siku ya Ijumaa walitia saini ya makubaliano ya kupiga jeki ushirikiano wao wa kiuchumi.
Uwekezaji wa Uturuki nchini Somalia unasimama zaidi ya dola milioni 100, Naibu Waziri Mkuu wa Kituruki amesema.
Aidha ametabiri kwamba kiasi cha biashara ya nchi hizo mbili itapanda hadi dola milioni 200 kutoka dola milioni 120 mwaka 2016.
Aliongeza wanatarajia biashara ya huru kati ya nchi hizo mbili ili kupiga jeki uhusiano wa biashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |