• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soka, CHAN 2018: Rwanda wapambana na Nigeria hadi mwisho 0-0

    (GMT+08:00) 2018-01-16 10:18:12

    Golikipa Eric ndayishimiye wa Rwanda jana amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupambana na hatari zilizokuwa zikiletwa langoni kwake na washambuliaji machachari wa timu ya Taifa ya Nigeria na kuupeleka mchezo wao wa kwanza wa kundi C la mashindano ya kombe la mataifa ya Africa kwa wachezaji wa ligi za ndani kuisha kwa matokeo ya sare ya bila kufungana.

    Licha ya umahiri wa Nigeria wa kumiliki mechi hiyo, vijana wa Amavubi wakiongozwa na Djihad Bizimana (aliyetangazwa mchezaji bora wa mechi) walimudu kuwianisha umiliki wa mpira kati ya pambe mbili hizo.

    Baada ya kuanza vizuri mechi hiyo, Rwanda sasa ili waweze kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele watalazimika kupata matokeo mazuri katika mechi ijayo watakapocheza na Equatorial Guinea siku ya alhamisi mjini Tangier.

    Katika mechi nyingine ya kundi C iliyopigwa jana Libya walishinda kwa magoli 2-0 dhidi Equatorial Guinea.

    Na michuano hiyo inaendelea leo kwa mechi mbili za kundi D zitakazopigwa mjini Agadir, ambako Angola watacheza na Burkina Faso, huku Cameroun dhidi ya Congo-Brazzaville.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako