China itaziruhusu kampuni zisizohusiana na nyumba na vijiji kujenga nyumba kwenye maeneo wanayoyamiliki ili kuboresha upatikanaji wa nyumba.
Mkutano wa kitaifa wa kazi za ardhi na rasilimali uliofanyika hapa Beijing umesema, jumla ya miji 13 ikiwemo Beijing, Shanghai, Nanjing, Hangzhou na Xiamen ni miji ya majaribio ambapo vijiji vinaweza kujenga nyumba za kupanga kwenye ardhi inayomilikiwa kwa pamoja, ya wao wenyewe au kwa ushirikiano na watu wengine.
Ardhi iliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba kwenye maeneo ya vijiji bado ni mali ya kijiji, na wakulima wataruhusiwa kuitumia kwa ujenzi wa nyumba na matumizi mengine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |