Shirika la kukadiria ubora wa bidhaa nchini Uganda UNBS limetaka kuondolewa mara moja sokoni kwa maziwa ya uanga ya watoto aina ya Picot, Milumel na Celi likisema bidhaa hizo zina vidudu vya Salmonela.
UNBS tayari imeifahamisha kampuni ya Lactalis Group ya Ufaransa inayotengeneza bidhaa hiyo kuhusu kuondolewa kwake na pia kuwatahadharisha wateja.
Mkuu w mawasiliano wa UNBS Godwin Bonge Muhwezi,amesema wanafanya ukaguzi kote nchini humo kuhakikisha bidhaa hiyo haiuzwi huku wakiendelea na uchuguzi zaidi ya mahabara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |