Hii ni mechi ya pili kwa Kenya ambao ni mabingwa wa Afrika, baada ya kucheza mechi ya kwanza jumapili iliyopita ambayo walifungwa na Afrika Kusini.
Kuelekea mechi ya Leo, kocha mkuu wa timu hiyo Jimmy Kamande, amesema tayari amefanyia kazi baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza katika mechi iliyopita, hivyo akitarajia matokeo mazuri katika mechi ya leo.
Kenya iko kundi A la mashindano hayo pamoja na timu za Afrika Kusini, New Zealand na mabingwa watetezi wa michuano hiyo West Indies.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |