• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soka, Klabu ya Yanga ya Tanzania yaingia ubia wa utengenezaji na uuzaji wa Jezi na kampuni ya Macron ya Italia

    (GMT+08:00) 2018-01-17 11:20:07
    Kampuni ya Macron yenye makao yake makuu nchini Italia imeingia mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya shilingi bilioni 2 na timu ya Yanga inayoshiriki ligi kuu nchini Tanzania kwa ajili ya utengenezaji na uuzaji wa jezi.

    Akizungumza baada ya hafla ya utiaji saini kwenye makao makuu ya klabu hiyo mjini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniphace Mkwasa amesema mkataba huo utakuwa na ongezeko kutokana na makubaliano waliyofikia na dau litakuwa likiongezeka kulinganana idadi ya mauzo ya jezi za mashabiki.

    Mkataba huu unakuja ikiwa ni mwezi mmoja baada ya kampuni ya Macron kusaini mkataba wa miaka miwili na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya udhamini wa jezi za timu zote za taifa za soka nchini Tanzania.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako