Satelaiti ya kwanza ya China ikiwa na wanafunzi wa shule za msingi na za kati wanaojihusisha na maendeleo na mchakato wa ujenzi itarushwa kwenye anga za juu ijumaa wiki hii.
Satelaiti hiyo iliyopewa jina la waziri mkuu wa zamani Zhou Enlai ilipelekwa kwenye kituo cha kurushia satelaiti cha Jiuquan kilichoko mkoa wa Gansu hapa China. Wanafunzi 20 walioshiriki kwenye maandalizi ya mradi huo walikwenda kwenye kituo hicho na watashuhudia satelaiti hiyo ikirushwa.
Msanifu mkuu wa satelaiti hiyo Zhang Xiang amesema, wanafunzi hao walitumia muda wao wa ziada kushiriki katika ujenzi na utendaji wa ardhini wa satelaiti hiyo, na walijifunza kuunganisha na kufanyia mazoezi data za sauti zinazosafirishwa na mfumo wa mawasiliano ya simu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |