Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amewaalika wafanyabiashara wa Zimbabwe walioko nchini Msumbiji kurudi nyumbani na kuwekeza nchini mwao, ambako uchumi unadidimia na unatakiwa uwekezaji mpya.
Rais Mnangagwa amesema hayo kwa jamii ya wafanyabiashara wa Wazimbabwe wakati wa ziara yake ya siku moja nchini Msumbiji, na kuongeza kuwa serikali yake inajitahidi kukabiliana na vikwazo vyote vya kisheria vinavyokwamisha biashara nchini Zimbabwe.
Naye rais Felipe Nyusi wa Msumbiji ameeleza kuunga mkono kauli ya rais Mnangagwa. Rais Felipe amewaambia wafanyabiashara hao wakipata nafasi wakaangalie fursa zilizoko nchini mwao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |