Halmashauri ya wanyama pori nchini Uganda inalenga kuinua mapato ya utalii mwaka huu kwa kuongeza juhudi ya kulinda wanyama pori.
Andrew Seguya mkurugenzi wa wa halmashauri hiyo amesema wawindaji haramu watachukuliwa hatua kali za kisheria mwaka huu baada ya kuanziswha kwa oparesheni koatika mbuga zote.
Mipango kadhaa ya kuimarisha utalii wa ndani aidha imeanzishwa baada ya ongezeko la asilimia 40 ya watalii mwaka jana.
Mwaka jana Uganda imepata watalii milioni 1.4 mwaka jana na juhudi hizo zinalenga kufikia milioni 2 mwaka huu.
Washikadau wametakiwa pia kuunga mkono vita dhidi ya uwindaji haramu unaopunguza idadi ya wanyama pori.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |