Mauzo ya magari nchini Kenya yamepungua kwa asilimia 20.3 mwaka jana kufuatia kudorora kwa uchumi.
Kampuni za Isuzu East Africa na Toyota Kenya zimeandikisha uniti ndogo zaidi za mauzo ikilinganishwa na mwaka juzi.
Mwaka juzi uniti 19,966 ziliuzwa ikilinganishwa na mwaka jana ambapo uniti za magari 11.044 pekee yaliuzwa.
Wauzaji magari wanalalamikia uchumi mbaya na utata wa kisiasa kuwa vyanzo vya kuporomoka kwa biashara ya magari.
Wadau wa magari wanatarajia ongezeko la asilimia 10 ya mauzo mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |