Rwanda yenye pointi moja kutokana na matokeo ya sare iliyopata ilipocheza dhidi ya Nigeria, inahitaji ushindi ili kujiweka katika mazingira mazuri zaidi ya kufuzu kwenda hatua ya robo fainali.
Mechi nyingine ya kundi C itakayopigwa leo Nigeria yenye pointi moja itacheza na Libya yenye pointi tatu.
Lakini safari ya wawakilishi wengine wa Afrika Mashariki, timu ya taifa ya Uganda itaishia hatua ya makundi kutokana na kufungwa tena katika mechi ya pili ilipocheza jana na Namibia kwa goli 1-0 mjini Marakech.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |