• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda yathibitishwa kuandaa michezo ya shule za sekondari za Afrika Mashariki mwaka huu.

    (GMT+08:00) 2018-01-19 09:02:23
    Nchi ya Rwanda imethibitishwa na shirikisho la vyama vya michezo kwa shule za Sekondari vya Afrika Mashariki (FEASSA) kuwa mwenyeji wa mashindano ya mwaka huu.

    Uthibitisho huo umekuja baada ya kukamilika kwa ukaguzi wa mji wa Musanze ambao ndiyo haswa utakuwa maskani ya michezo hiyo mwezi Agosti.

    Timu ya wakaguzi ilijumuisha wawakilishi kutoka nchi za Tanzania, Uganda, Kenya na Rwanda ikiongozwa na Rais wa FEASSA Justus Mugisha.

    Rwanda ambayo inaandaa michezo hiyo kwa mara ya pili ikiwa imewahi kufanya hivyo mwaka 2015, inatarajia kupokea wanamichezo 4000 (wakiwa ni wachezaji na viongozi) kutoka nchi sita za Kenya, Burundi, Tanzania, Uganda, Sudan Kusini na Rwanda.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako