Waziri wa mambo ya ndani wa Burundi amesema kampeni ya kufafanua marekebisho ya katiba ya Burundi kabla ya kura za maoni zitakazofanyika mwezi Mei mwaka huu, inaendelea vizuri.
Serikali ya Burundi imesifu jinsi kampeni hiyo inavyoendelea nchini kote. Ripoti kutoka mikoani na wilayani zinaonyesha kwamba wananchi wanaelewa hatua kwa hatua mabadiliko yaliyoko kwenye rasimu ya katiba.
Mwezi Desemba mwaka jana, tume ya uchaguzi ya taifa ya Burundi ilitangaza kuwa kura za maoni kuhusu katiba zitafanyika mwezi Mei mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |