Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China CPC imependekeza kuandika Fikra ya Xi Jinping kuhusu Ujamaa wenye Umaalumu wa Kichina katika Kipindi Kipya kwenye Katiba.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye kikao cha pili cha wajumbe wote cha Kamati Kuu ya CPC, kilichofanyika jana na leo hapa Beijing, mafanikio makubwa ya kidhana, kanuni na sera zilizopitishwa katika Mkutano Mkuu wa 19 wa CPC zinapaswa kujumuishwa katika marekebisho ya Katiba yatakayofanyiwa baadaye.
Pendekezo lililotolewa na Kamati Kuu ya CPC kuhusu marekebisho hayo ya Katiba limepitishwa katika mkutano huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |