Sudan na Morocco zilizokuwa tayari zimefuzu, ziliingia uwanjani kusaka timu itakayokuwa vinara wa kundi A baada ya zote kuwa na pointi zinazolingana, hata hivyo nafasi kubwa ilikuwa kwa Morocco ambao wana wastani mkubwa wa magoli.
Timu zote zilishambuliana bila ya mafanikio, lakini zaidi fursa ilijitokeza kwa Morocco ambao walizawadiwa penati ambayo golikipa wa Sudan El Hadi Salum aliipangua.
Leo ni zamu ya mechi za kundi B, ambapo timu za Namibia na Zambia zitacheza kutafuta kinara wa kundi baada ya zote kulingana kwa pointi, lakini Uganda na Ivory Coast zitacheza kwa ajili ya kukamilisha ratiba kwa kuwa zote zimekwisha shindwa kufuzu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |