Rwanda watashuka dimbani leo mjini Tangier kucheza na mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Libya katika mechi yao ya mwisho kwenye hatua ya makundi.
Ushindi ni lazima kwa Rwanda ili kusonga mbele, licha ya kuwa sare itawafaa endapo Nigeria wataifunga Equatorial Guinea katika mechi nyingine ya kundi C itakayopigwa muda huo huo mjini Agadir.
Kocha mkuu wa Rwanda Antoine Hey ameweka wazi kuwa mchezo huo, hautakuwa mrahisi isipokuwa watapambana ili kufuzu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |