Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Freddy Liundi, alisema ufanisi huo upo pia katika mizigo mingine, yakiwemo makasha.
Liundi alisema kwa sasa bandari yao inafanya vizuri, kuanzia upakuaji na utoaji wa makasha pamoja na magari kulinganisha na hali ya utendaji ilivyokuwa kwa miaka ya nyuma.
Alisema wanajitahidi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, lakini wakati mwingine matatizo yanayotokea husababishwa na wadau wao wanaoshirikiana nao kupokea na kusafirisha mizigo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |