• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya-Ujenzi wa  kituo cha umeme katika bandari ya Mombasa

    (GMT+08:00) 2018-01-24 19:21:08

    Halmashauri ya bandari nchini Kenya (KPA) inatarajia kujenga kituo cha kusambaza umeme kwa meli zinazoingiza mizigo katika bandari ya Mombasa ili kupunguza uharibifu wa mazingira ya bahari.

    Bandari ya Mombasa haina kituo cha kusambaza umeme katika eneo la meli kutia nanga bandarini na kusababisha meli kuacha injini zikinguruma na kutoa moshi mwingi.

    Mkuu wa kituo cha Maritime Technology Cooperation Centre (MTCC) Africa,mhandisi Michael Muchiri amesema ujenzi wa kituo hicho utagharimu Sh150 milioni.

    Muchiri amesema ujenzi wa kituo cha kusambaza umeme katika meli zinazoleta mizigo bandarini ni muhimu kwa kuwa kitawezesha kupunguza kiwango cha moshi unaotoka katika meli ambao hudhuru mazingira ya bahari.

    Ujenzi huo wa kituo hicho utawezesha bandari kusambaza umeme kwa meli za mizigo kuzima injini ili kukabili athari za moshi wenye gesi ambazo hudhuru mazingira ya bahari.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako