Mkurugenzi mkuu wa klabu hiyo Bw. Ed Woodward amesema wameamua kumuongeza Mourinho mkataba kutokana na mafanikio aliopata katika msimu wake wa kwanza kitu ambacho hakuna kocha mwingine ambaye amewahi kufanya hivyo.
Upekee wa Mou ni kwamba, aliweza kutwaa kombe la EFL mwezi Februari mwaka jana, pia alitwaa kombe ambalo hakuna kocha mwingine aliwahi kulinyakua katika historia ya klabu ambalo ni kombe la Yuropa jijini Stockholm.
Woodward pia amekiri kuwa tangu Mourinho atue United, amerejesha imani, ameongeza ari na motisha kwa mashabiki na klabu kwa ujumla.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |