Timu ya waendesha baiskeli kutoka Rwanda, jana imesafiri kwenda nchini Cameroun kwa ajili ya kushiriki mashindano ya kimataifa ya Baiskeli ya vijana chini ya miaka 23 yanayoanza rasmi Januari 31.
Bingwa wa Afrika Joseph Areruya anatarajiwa kuongoza timu hiyo katika mashindano hayo yanayoandaliwa shirikisho la mchezo wa baiskeli la Cameroun na shirikisho la vyama vya baiskeli vya kimataifa.
Timu zingine zinazoshiriki mashindano hayo ya siku nne ni South Africa, Algeria, Burkina Faso, Ivory Coast, Egypt, Eritrea, Ethiopia, Mali, Morocco, Mauritius, Democratic Republic of Congo, Tunisia and hosts Cameroon.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |